header

nmb

nmb

Monday, January 16, 2012

MSIBA WA MBUNGE WA VITI MAALUM WA CHADEMA,MH. REJIA MTEMA,RAIS KIKWETE ATEMBELEA NYUMBANI.








Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro kupitia tiketi ya CHADEMA, Mh. Rejia Mtema lipataata ajali eleo la Ruvu na kufariki dunia papo hapo. Mh. Mtema alikuwa akisafiri kuelekea Mkoani Morogoro.


Kwa Mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo walisema kuwa mbunge huyo ambaye alikuwa akiendesha mwenyewe gari lake amepinduka na gari hilo mara baada ya kumshinda wakati akijaribu kulipita gari lililokuwa mbele yake katika eneo hilo la Ruvu.


Ndani ya Gari hilo kulikuwa kuna watu wengine wanne.Taarifa zaidi zinasewma kuwa Mipanga ya mazishi inaendelea na wanatarajia kuzika kesho kijijini kwao mkoani Morogoro




Rais Jakaya Kikwete akijiunga na waombolezaji katika msiba wa Mbunge wa Viti Maalumu (CHADEMA) Mh Regia Mtema leo January 15, 2012 nyumbani kwa marehemu Tabata jijini Dar es salaam ambako Waziri Mkuu Mh Mizengo Pinda, Spika Anne Makinda na Mwenyekiti wa CHADEMA Mh Freeman Mbowe walikuwapo.


PICHA NA IKULU

Rais Jakaya Kikwete akiwafariji wafiwa katika msiba wa Mbunge wa CHADEMA Mh. Regia Mtema leo.

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mwenyekiti wa Chama Cha CHADEMA Mh Freeman Mbowe wa tatu kutoka kulia pamoja na jamaa wa Marehemu Regia Mtema.

Rais Jakaya Kikwete akiteta jambo na Waziri Mkuu Mizengo Pinda katikati pamoja na Spika wa Bunge Mh. A

No comments:

Post a Comment