header

nmb

nmb

Thursday, September 8, 2011

WATANZANIA TUTEGEMEE NINI KUTOKA KWA MWANAFUNZI ANAYEMALIZA ELIMU YAKE YA MSINGI KWA KUFANYA MTIHANI WAKE WA MWISHO KATIKA MAZINGIRA HAYA!

Wanafunzi wa Darasa la Saba wakifanya Mtihani wao wa kumaliza Elimu ya msingi leo.

Watanzania Elimu yetu ipo wapi na inakwenda wapi! hili ni swali ambalo lazima wengi wetu tutakua tunajiuliza.
Hali kama hii kwa wanafunzi kufanya Mtihani wa mwisho wakiwa wamekaa chini itaisha lini! ni jambo la kusikitisha sana hali kama hii inavyoendelea na naona kama inazidi kuota mizizi, wahusika wako wapi; Wizara ya TAMISEMI wapo wapi? Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi wapo wapi?

Hizi Wizara zinataka Mtanzania wa kesho awe na Elimu ipi ambayo inaweza kumkwamua katika haya maisha ya leo na mbeleni ambayo mwenye elimu ndio atakayetambulika

KAPINGAZ Blog inawaomba wahusika wote ambao wanahusika katika kuboresha Elimu za watoto wetu waliangalie hili katika mtazamo mpana zaidi, sidhani kama tutaweza kuwapata wanasayansi wazuri kwa kuwafanyisha Mitihani katika hali hii.

Karne tulionayo ni ya kumpa Mwanafunzi "ELIMU BORA SIO BORA ELIMU

zaid bofya humu
http://kapingaz.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment