header

nmb

nmb

Wednesday, May 26, 2010

Brazil kukipiga na Taifa Starz kabla ya Kombe la Dunia...!



Shirikisho la soka nchini TFF limethibitisha ujio wa timu ya taifa ya BRAZIL kwa ajili ya mchezo wa kirafiki na timu ya taifa ya TANZANIA TAIFA STARS kabla ya kwenda Afrika Kusini.

Rais wa TFF LEODGAR TENGA amesema kuwa Tanzania imepokea kwa furaha ombi la nchi ya Brazil hivyo kwa sasa mazungumzo bado yanaendelea kuhusiana na ujio wa timu hiyoAidha Tenga amesema kuwa ujio wa Brazil unahitaji maandalizi makubwa hivyo juhudi kubwa inafanyika ili serikali itoe msaada mkubwa kwa ujio wa timu hiyo namba moja katika viwango vya soka Duniani.

Brazil itacheza michezo ya kirafiki na TANZANIA pamoja na ZIMBABWE, kabla ya kwenda nchini AFRIKA KUSINI kwa ajili ya michuano ya kombe la dunia.
michezo hiyo itachezwa June 2 na 7 kabla ya BRAZIL haijacheza mchezo wake wa kwanza wa fainali za kombe la dunia dhidi ya KOREA KASKAZINI june 15.
Hivi sasa BRAZIL ipo nchini mwake katika jiji la CURITIBA lililopo kaskazini mwa nchi hiyo wakiendelea na mazoezi.

No comments:

Post a Comment