header

nmb

nmb

Sunday, June 10, 2012

Miss Chang'ombe huyuhapa!!
Redds Miss Chang’ombe 2012, Catherine Masumbigana 21, (katikati) akipunga mkono mara baada ya kusimikwa rasmi kuwa mshindi wa taji hilo. Kulia ni mmshindi wa pili, Jesca Haule (18) na Mshindi wa tatu Zulfa Bundala. Masumbigana aliwashinda warembo wengine 13 katika shindano hilo lililofanyika katika Ukumbi wa Quality Center jijini Dar es Salaam Juni 10, 2012.

 Tano bora ya Miss Chang’ombe 2012 ambao wote wamepata tiketi ya kushiriki shindano la Miss Temeke 2012 wakiwa katika picha ya pamoja. Kutoka Kushoto ni Zulfa Bundala (21), Jesca Haule (18), Catherine Masumbigana (21), Miriam Nkisigwa (20) na Flora Kazungu.
 Warembo wakicheza show maalum ya ufunguzi

 Vazi la ufukwenu, Kutoka kulia ni Restituta Faustiney, Wensley Mabula na Clara Diu.
 Warembo Flora Mayasa (kulia) Catherine Masumbigana (katikati) na Elizabeth Mushi wakiwinda point na vazi la ufukweni.
Mkali wa Bongo Fleva Nassib Abdul 'Diamond' na vijana wake walisindikiza show hiyo kwa kutoa burudani kali jukwaani.
 Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Vijana (Mb) Amos Makala akizungumza jukwaani.
 Wapenzi wa urembo kutoka Chuo Kikuu cha Kampala tawi la Dar es Salaam nao walikuwepo.
 Washiriki wa Miss Ilala 2012 kutoka Kitongoji cha Tabata jijini Dar es Salaam nao hawakukosekana

BREAKING NEWSSSSSSSSSSSS:PROFESA GEORGE SAITOTI AFARIKI KATIKA AJALI YA HELIKOPTA NCHINI KENYA


 Waziri wa Usalama wa ndani wa Kenya Profesa George Saitoti amefariki dunia kwa ajali ya Helikopta iliyotokea leo asubuhi katika eneo la Ngong Katika milima ya Magharibi mwa Nairobi nchini humo wakati akiwa katika safari ya kikazi akielekea Kisumu, Saitoti amefariki akiwa na Naibu Waziri wake Orwa Ojode.
Mbunge wa Kenya Najib Balala amethibitisha kutokea kwa kifo hicho katika mtandao wake wa Twitter, Serikali ya Kenya bado haijasema chochote kuhusu sababu za ajali hiyo iliyopoteza mawaziri hao pamoja na watu wengine wanne jumla yao wakiwa Sita, Profesa Saitoti alikuwa akitarajia kugombea urais katika uchaguzi wa Rais utakaofanyika baadae mwaka huu

No comments:

Post a Comment