header

nmb

nmb

Wednesday, September 14, 2011

TIMU ZA SIMBA NA YANGA ZIMEJIFUNZA NINI KUTOKA KWA AZAM FC!

Logo ya Timu ya Simba Sports Club al-maarufu kama wekundu wa Msimbazi.

Logo ya Timu ya Yanga Africans al-maarufu kama watoto wa Jangwani.

Logo ya Timu ya Azam FC

Napenda niwaulize wadau kama kweli ni haki kwa Timu za Simba na Yanga kuufanya uwanja wa Azam FC kuwa kama uwanja wao wa nyumbani!! La hasha, kwa mimi nitasema si haki, ni kitendo cha aibu sana kwa timu hizi mbili kubwa ambazo kama tunavyoona hapo kwenye Logo zao zinaonyesha ni jinsi gani zilivyo vilabu kongwe hapa nchini lakini havina viwanja vyao vya kuweza kucheza mechi zao za ligi za nyumbani na za kimataifa.

KAPINGAZ Blog inawaomba Viongozi wa timu hizi mbili mlio madarakani kwa sasa muone hili ni kama changamoto kwenu kwa timu changa imeweza kuwa na uwanja wake, na timu zenu zikajikuta mnaenda kucheza kwenye uwanja huo, ni fedheha sana kwenu.
"USHAURI WA BURE VIONGOZI JITAHIDINI KUJALI MASLAHI YA TIMU"

No comments:

Post a Comment