Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Dr. Patrick James Makungu amezindua huduma mpya ya Tigo Pre Paid Blackberry leo kwenye uzinduzi uliofanyika kwenye hotelia ya Kilimanjaro Kempinski jijini Dar es salaam.
Akisoma hotuba yake katibu mkuu huyo amesema"Ninayo furaha kubwa kuwa nanyi mchana huu wa leo ambapo Tigo mnazindua huduma yenu kabambe ya malipo ya kabla ya mtandao wa intanet ya backberry kupitia mtandao wa Tigo – Tigo Pre paid blackberry Kwa niaba ya serikali kupitia wizara mawasiliano sayansi na teknolojia kwanza niwapongeze kwa hatua hii nzuri mliofikia ya kuamua kuleta huduma hii ya blackberry malipo ya kabla ambayo kama mlivyosema mmeitikia ombi toka kwa wateja mnaowahudumia Pili ninawapongeza kwa kuweka vifurushi vya viwango vya chini zaidi na nafuu kuliko mtandao wowote nchini katika huduma hii ya backberry malipo ya kabla
No comments:
Post a Comment