header

nmb

nmb

Monday, September 20, 2010

PSI SERIKALI YAWAANZISHIA VIJANA TAMASHA LA KUPIGA VITA V .V.U!!



PSI yazindua michezo kuhamasisha vijana kupima VVU
Na Peter Mwenda
SHIRIKA lisilo la Kiserikali la PSI kushirikiana na Serikali wameanzisha mradi kutumia michezo na burudani kuhamasisha vijana kupata elimu kuhusiana na ugonjwa wa Ukimwi na VVU.
Akizindua mradi huo jana,Ofisa Afya wa Manispaa ya Temeke,Dkt. Silvia Mamkwe katika viwanja vya Mbagala kwa michezo mbalimbali alisema vijana watajitambua afya zao kwa kupima.
Alisema michezo ni sehemu ya kuimarisha miili na kujenga afya pia ikitumika kuelimisha vijana kupima afya zao ukimwi utakwisha Tanzania.
Katika burudani hizo vijana walishindana kupambana katika mpira wa miguu, kufukuza kuku,riadha na mpira wa kikapu.
Ofisa Uhusiano wa PSI, Gaston Shayo aliambia majira kuwa mradi huo utaendelezwa na kufanyika nchini kote ambako vijana zaidi ya 600,000 wanatarajiwa kupata elimu hiyo.
mwisho.










Mashabiki wa timu ta soka ya Vikuruti FC ya Maji Matitu Mbagala Dar es Salaam wakiwa wamembeba mchezaji wao Mussa Kumra baada ya Kufunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penalti na kuifunga Maji Matitu FC kwa Mabao 3.2 katika fainali ya Kombe la PSI. Mchezao huo umeandaliwa kuhamasisha vijana kujikinga na VVU (Ukimwi).Tamasha hilo liliandaliwa na Serikari kwa Kushilikiana na PSI(Picha na Spear Patrick)
KAMBA
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Maji Matitu Mbagala wakivuta kamba wenzao wa Shule ya msingi ya Mbagala wakati wa Tamasha la Kuhamasisha Vijana kujikinga na VVU (UKIMWI) lililofanyika Maji Matitu Dar es Salaam.Tamasha hilo liliandaliwa na Selikari kwa Kushilikiana na PSI .
KIGWENDU
Msanii wa Muziki na Vichekesho Rashidi Mzangwe Maarufu Kingwendu akiwana Kundi wake wakicheza muziki wakati wa Tamasha la Kupiga vita Maambukizi ya VVU (UKIMWI) mbagara Maji matitu Dar es Salaam jana.Tamasha hilo liliandaliwa na Selikari kwa Kushilikiana na PSI. (














No comments:

Post a Comment