header

nmb

nmb

Tuesday, September 21, 2010

ALIYE DAI KUTOROSHEWA MKE NUSURA AUWAWE NA WATU WASIO JULIKANA NYUMBANI KWAKE USIKU WA MANANE!!

Amanuel Chadiel Mahimbo mkazi wa Kimara, Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, anayedai kuporwa mke na mgombea Urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbroad Slaa amekumbwa na masaibu mapya kwani amevamiwa na watu wasiojulikana nyumbani kwake, usiku wa manane baada ya kutimuliwa katika nyumba ya kigogo aliyokuwa amejificha.

Amanuel Chadiel Mahimbo anayedai kuporwa mke.
Taarifa zilizofikia katika mtandao wa Global publishers siku chache baada ya kuandika habari kuhusu kutoweka kwake na kuhamia kwa kigogo huyo kufuatia kupigiwa simu za kumtishia maisha yake, rafiki wa Mahimbo (jina linahifadhiwa) alisema alipewa taarifa na mhusika kuwa nyumbani kwake Kimara kulivamiwa na kundi la watu wasiofahamika usiku wa manane.

“Watu hao walimkuta mlinzi wake ambaye ni Mmasai na kumuulizia Mahimbo alipo lakini wakaambiwa hayupo na hajaonekana siku kadhaa, walimtia kashkash, wakaondoka”, alisema rafiki huyo.habari kwa hisani ya Mtandao wa Global Publishers.Zaidi Tembeklea upate Uhondo nzima
Dk. Willbroad Slaa.

No comments:

Post a Comment