header

nmb

nmb

Tuesday, September 21, 2010

Precision Air yazidi kuchanja mbuga yazindua dege jingine!!

Shirika la Ndege Binafsi nchini leo imezindua ndege yake ya saba mpya aina ya ATR 72-500 katika sherehe iliyofanyika katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere-Terminal Two jijini Dar es Salaam.

Uzinduzi wa ndege hiyo uliongozwa na Mwenyekiti wa IPP media Bw. Reginald Mengi kama mgeni rasmi na kuhudhuriwa pia na mabalozi, wadau wa biashara wa Precision Air pamoja na wafanyakazi wa shirika la ndege hilo.

Mkurugenzi Mkuu na Meneja

Mwendeshaji wa Precision Air, Bw. Alfonse Kioko alisema, “Mpango wetu wa kuongeza idadi za ndege ni mkakati madhubuti kabisa katika ukuaji wa kampuni na kutimiza huduma iliyo bora kwa wateja.”

Aliendelea: “Kutimia kwa ndege hizi mpya saba ni kuongezea nguvu ndege zetu tatu za zamani, kitu ambacho itatuwezesha kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuweza kutimiza mahitaji ya wateja wetu kwa gharama nafuu zaidi. Hii ni kwa manufaa yetu sote, sisi na wateja wetu.”

Ndege hii mpya iliwasili tarehe 18 Septemba 2010 kutokea Toulouse-Ufaransa ambapo makao makuu ya ATR na kiwanda cha ndege kilipo. Ndege hizi aina ya ATR zimetengenezwa mahususi kabisa kwa namna ambayo madhara yake kwa mazingira na ya hali ya hewa ni mfinyu mno, kwa maana utoaji wake wa gesi aina ya kaboni ni mdogo. Hakika hii ni hatua na chaguo la kipekee kabisa kwa Precision Air kujali mazingira.

Zaidi Bofya hapa FULLSHANGWE.BLOGSPOT.COM

No comments:

Post a Comment