header

nmb

nmb

Friday, September 24, 2010

Mustafa Hassanali kuwa mgeni rasmi onyesho la mavazi mjini arusha.



Wakazi wa Arusha kumuona Mustafa Hassanali live

Ni mgeni rasmi katika Onyesho linalofanyika New Arusha Hotel

Visura 10 kuonesha mavazi yaliyooneshwa na Mustafa Hassanali nchini Cameroon February na Zanzibar Julai 2010.


Mwanzilishi na muandaaji wa jukwaa la wanawake wajasiriamali Tanzania (TWENDE ) na Jukwaa la kukuza vipaji vya wabunifu chipukizi Swahili Fashion Week, ambae pia ni mbunifu maarufu wa mavazi, Mustafa Hassanali amealikwa kuwa mgeni rasmi katika maonyesho ya mavazi yanayofanyika jijini Arusha kwa muda wa siku mbili tarehe 23 na 24 ya mwezi huu katika hoteli ya New Arusha.


Maonyesho hayo yameandaliwa na Maridadi. Maridadi ni kikundi kinachojumisha wanawake watatu kutoka mataifa tofauti ya Tanzania, Austarialia na Uholanzi ambao wanaishi nchini katika jiji la Aruha na kujishughulisha na masuala mbalimbali yanayohusiana na mendeleo ya mwanamke.


Akielezea lengo la kuandaa maonyesho hayo, mmoja wa wanawake hao, Lilian Bulengo amesema kuwa “dhumuni kuu la kuandaa tukio hili linalojulikana kwa jina la “Maridadi Women Show” ni kuwakutanisha pamoja wanawake kutoka maeneo tofauti ya Arusha na Moshi katika Fashion Show, maonyesho ya biashara pamoja na kupata fursa ya kuzungumza mambo mbalimbali yanayowakabili wanawake katika maisha ya kila siku hapaTanzania ikiwemo suala la unyanyasaji wa kijinsia na ubakaji, wanawake na kuondokana na utegemezi na masuala ya uchumi na biashara kwa ujumla”.

.

KAMA UMENOGEWA TEMBELEA MICHUZI JR IONE KWA UNDANI


Pili Pili Entertainment wazindua filamu mpya ya black sunday usiku huu.

Mkurungenzi wa kampuni ya Pili Pili Entertainment (katikati) Sameer Srivastava akimpongeza nyota mmojawapo wa filamu mpya iliozinduliwa usiku wa leo iitwayo Black Sunday,ndani ukumbi wa cinema wa Mlimani City,Steven Kanumba kwa kuonyesha umahiri wake mkubwa wa kuigiza ndani ya filamu hiyo iliokuwa na msisimko mkubwa kwa watazamaji. Mbali ya Kanumba pia kulikuwepo na nyota wengine walioinogesha filamu hiyo vyema kama vile Aunt Ezekiel,Monalisa,Yusuph Mlela na wengineo.Uzinduzi wa filamu hiyo uliandaliwa na kampuni ya Pili Pili Entertainment na kuhudhuriwa na wageni waalikwa mbalimbali.
Nyota wa filamu ya Black Sunday iliozinduliwa usiku wa leo,Steven Kanumba akibadilishana mawazo na baadhi ya wageni waalikwa waliofika kwenye uzinduzi wa filamu hiyo iliokuwa na waigizaji wenye vipaji kibao, mara baada ya kutoka kuitazama.
Wageni waalikwa wakiingia kwenye ukumbi kuishuhudia filamu hiyo usiku huu.
Wadau mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuingia ndani ya ukumbi husika kuishuhudia filamu hiyo ya Black sunday,ambayo kiukweli imejawa na matukio ya kusisimua mno.
Pichani kushoto ni mdau Hala hala akiwa amepozi na Mkurungenzi wa kampuni ya Pili Pili Entertainment (katikati) Sameer Srivastava pamoja na Mdau mwingine wa mambo ya filamu.
Slyvia na rafiki yake wakiwa wamepozi mbele ya kamera ya Jiachie usikuu
Wadau wakitoa mawazo yao mbalimbali kabla ya kwenda kuitazama filamu yenyewe..MAPICHA NA HABARI ZAIDI MICHUZI JR

No comments:

Post a Comment