Katika tukio hilo la wiki iliyopita,Nyombi alivithibitishia vyombo vya habari kuwa Barick aliwahi kufungwa miaka mitatu jela na kuachiwa April 26, mwaka huu, ambapo alhamisi iliyopita,alikaririwa akisema kuwa majambazi hayo yaliuawa Juni 3, mwaka huu majira ya usiku.
Kamanda Nyombi alikaririwa akisema kuwa polisi walipokuwa katika doria yalifanikiwa kuyanasa majambazi hayo baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema kuwa yalikuwa yakiwavizia wafanyabiashara wa mbao katika Barabara ya Katumba kijijini hapo. Aidha Kamanda Nyombi aliwataja majambazi waliouawa katika tukio lililotokea wilayani Rungwe waliotambuliwa kuwa ni Maneno Mtasiwa(30) Mkazi wa Block Q jijini hapa na Mfanyabiashara wa Viatu vya Mitumba katika Soko la Mwanjelwa, Zawadi Pamelo (32) na Mmoja aliyetambuliwa kwa jina la Benny Makazi wa Nzovwe jijini hapa. Hata Hivyo Kamanda Nyombi aliwataja watuhumiwa wengine wanaoshikiliwa na Jeshi la Polisi ambao wanadaiwa kukimbia katika majibizano ya risasi na polisi kuwa ni Edson Mabisa(30)ambaye alikamatwa katika daraja lilipo katika jirani na Stendi kuu ya mabasi yaendayo mikoani ikiwa pamoja na Ally Mohamed (30) ambao wote ni wakazi wa mji mdogo wa Tunduma.
No comments:
Post a Comment