header

nmb

nmb

Friday, June 18, 2010

RISASI ZAWATIAHOFU WAKAZI WA MUSOMA WAHOFU UGAIDI!!


HOFU kubwa ilitanda jana kwa wakazi wa Manispaa ya Musoma mkoani Mara baada ya askari kurusha risasi hovyo hewani ili kuweza kumkamata mshtakiwa aliyetoroka akiwa chini ya ulinzi.
Tukio hilo lilitokea saa 5.30 asubuhi ambapo mtuhumiwa huyo alikuwa katika Mahakama ya Mkoa kwa ajili ya kusikiliza kesi iliyokuwa inamkabili.
Mtuhumiwa huyo ambaye jina lake halikujulikana mara moja wala kosa lake aliokuwa akikabiliwa nalo alikamatwa kwa msaada wa askari kutoka kituoni akiwamo askari wa usalama barabarani.
Katika tukio hilo, polisi iliwachukua muda kadhaa hadi kumkamata mshtakiwa na kulazimika kurushwa risasi hewani hali iliyosababisha wananchi mbalimbali wilayani humo kukimbia hovyo na wengine kuzirahi kutokana na milio ya risasi.
Tukio hilo lilitendeka karibu na ofisi kuu ya Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Musoma, ofisi za mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) na ofisi za RPC.
Kamishna Mwandamizi wa Polisi Mkoa huo, Robert Boaz hakuweza kupatikana kwa njia ya simu ili kuzungumzia tukio hilo.
“Inaonekana walimbamiza kichwa chake ukutani,” alisema Malefo. “Baada ya kumjeruhi vibaya waliwapigia simu lakini wakati polisi walipowasili tayari mwanamume huyo alikuwa amekufa.” aliongeza msemaji huyo wa Polisi.
Maleto alisema wote watatu walikamatwa Jumapili usiku na kuswekwa rumande lakini Lebogang aliachiwa Jumanne kwa dhamana ya dola 200 na wengine wawili bado wanashikiliwa rumande.
Kamanda Malefo alisema kuwa mama na wanaye hao wawili wanatarajiwa kufiukishwa mahakama ya Seshego Julai 27 mwaka huu.
“Mara zote alikuwa mchangamfu na hakuwa mtu wa fujo,” majirani wa Makoeya, Miriam na Anna, waliliambia gazeti la Daily Sun la Afrika Kusini. “Kwa mara ya mwisho tulionana naye Jumamosi kwenye mazishi,” waliongeza majirani hao.
Fainali za Kombe la Dunia zinafanyika barani Afrika kwa mara ya kwanza na zilianza kutimua vumbi tangu Ijumaa wiki iliyopita na zitaendelea hadi Julai 11 mwaka.Zaidi pata Dar Leo ya Leo

No comments:

Post a Comment