header

nmb

nmb

Friday, June 18, 2010

MADENTI WALIO BAKWA NA KUIBIWA WAPATA FARAJA. NI BAADA YA KOVA KUWAKAMATA WABAKAJI HAO!!



JESHI la Polisi nchini limewanasa watu waliovamia, kubaka na kisha kuiba mali mbalimbali za wanafunzi wa Chuo Cha Uandishi wa Habari (DSJ) kilichopo Ilala Sharif Shamba jijini Dar es Salaam.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu Mkoa wa Dar es Salaam, Suleimani Kova, amesema watuhimiwa hao walikamatwa jana katika msako mkali uliofanywa na askari wa upelelezi.
Madenti wa chuo cha huko majuu wakiigiza tukio hilo.Amesema baadhi ya watuhumiwa walikamatwa usiku wa kuamkia leo wakiwa kwenye gari namba T 987 KYJ aina ya Honda na gari nyingine ni T 870 ATD aina ya Toyota Cresta.
Amesema baada ya upekuzi walifanikiwa kuwakuta watuhumiwa wakiwa na marungu, bisibisi, nyundo, na funguo bandia katika Mtaa wa Mafia.
Amesema watuhumiwa waliokamatwa ni Haruni Abdani, Hamisi Juma (24), Ally Msesa (34) mkazi wa Sinza, Abdul Selemani (27) na Abdu Mariki (26).
Amesema katika uchunguzi wa awali wamebaini kuwa washtakiwa hao walihusika katika tukio hilo kutokana na kukutwa na silaha hizo.
Kamanda Kova amesema bado uchunguzi zaidi unaendelea kuhusiana na tukio hilo.Aidha amewaomba wananchi kutoa taarifa kwa siri pindi wanapomuhisi mtu kuhusika na tukio hilo.Zaidi Nunua Dar leo ya leo

No comments:

Post a Comment