header

nmb

nmb

Thursday, February 7, 2013

DAMPO LA SOKO LA KIHESA LILILOKUWA KERO KWA KUTUPWA MIZOGA YA MBWA ,LAFANYIWA USAFI

 

Mkazi  wa  Kihesa ambae ni mfanyabiashara  wa soko  la Kihesa akionyesha dampo ambalo jana mtandao huu uliripoti kuwa ni chafu na takataka  zimejaa pamoja na kutupwa mbwa wanne  waliouwawa mitaani .

Leo uongozi  wa afya Manispaa ya Iringa  umefika  kuondoa taka ndani ya dampo hilo na kufanya eneo hilo  kurejea katika hali ya kawaida ya usafi japo  wameomba Manispaa ya Iringa isingoje hadi  watu  walalamike ndipo taka zitolewe katika vituo.

Mtandao  huu  wa www.francisgodwin.blogspot.com unaupongeza uongozi  wa afya manispaa ya  Iringa kwa  kushughulikia tatizo hilo kwa  wakati .

HII NDIO STORI YENYEWE YA JANA NDANI YA MTANDAO HUU

WATEJA SOKO LA KIHESA WAKIMBIA HARUFU KALI YA MIZOGA YA MBWA WANAOTUPWA KWENYE DAMPO SOKONI HAPO

 Mbwa  waliouwawa na maofisa  wa mifugo Manispaa ya Iringa  wakiwa  wametupwa katika dampo la taka  eneo la soko la Kihesa na kupelekea wateja  kukimbia katika  soko  hilo kwa harufu kali ya mizoga hiyo ya mbwa
 Mfanyabiashara  wa soko la Kihesa akionyesha mzoga wa mbwa uliotupwa  katika dampo hilo baada ya  kuuwawa na maofisa mifugo wa Manispaa ya Iringa ,huku chini kukiwa na mzoga mwingine wa mbwa uliotupwa eneo hilo ambalo zaidi ya mbwa wanne wametupwa jana na leo
Dampo  likiwa na taka pamoja na mbwa  waliotupwa eneo hilo .

No comments:

Post a Comment