Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na 
Michezo Mhe.Nape Moses Nnauye amemtangaza Bw.Hassan Abbas kuwa 
Mkurugenzi wa Idara ya Habari MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali 
kuanzia Agosti 5 Mwaka huu.
Uteuzi huo umefanyika kwa mujibu wa 
Sheria za Utumishi wa Umma Namba 8 ya mwaka 2002 kifungu Namba 6(1)(b) 
kufuatia uhamisho wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara hiyo Bw. Assah 
Mwambene uliofanyika tarehe 7 Machi 2016 kwenda Wizara ya Mambo ya Nje 
na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Mhe.Nape Moses Nnauye ametoa wito kwa 
Wanahabari na Wananchi kwa ujumla kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Bw 
Abbas atakapokuwa anatekeleza majukumu yake.
“Ninawaomba Wanahabari na Watanzania 
kwa ujumla mumtambue Bw Abbas na mtoe ushirikiano unaostahili katika 
utendaji wa kazi zake”.Alisema Mhe. Waziri.
Aidha Mhe. Waziri Nape alimpongeza 
Bibi Zamaradi Kawawa aliyekuwa anakaimu nafasi hiyo kwa kujituma na 
kusimamia majukumu yote ya Idara kwa ukamilifu na uadilifu.
Kwa upande wake Mkurugenzi huyo mpya 
amekubali uteuzi huo na ameahidi kuitumikia nafasi hiyo kwa uadilifu 
mkubwa na ameomba ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wafanyakazi wa Idara
 ya Habari Maelezo na Watanzania kwa ujumla.
Kabla ya uteuzi huo Bw. Hassan Abbas 
alikuwa ni Meneja Habari na Mawasiliano katika Ofisi ya Rais 
inayosimamia Utekelezaji wa Program ya Matokeo Makubwa sasa (President`s
 Delivery Bureau).
 
 



 
 
No comments:
Post a Comment