header

nmb

nmb

Tuesday, October 1, 2013

AFRICA CETRE FOR PEACE AND CONFLICT RESEARCH - ACPCR





Kituo cha Amani na utafiti wa migogoro Africa kilianzishwa mwaka 2012 na wataalamu wa Masuala ya Amani ya Kimataifa na utafiti wa migogoro ambao ni wahadhiri wa vyuo vikuu. Wahadhri hao pamoja na wanafunzi wa fani hii ya amani wameguswa na jinsi ambavyo Bara la Africa limekumbwa na kugawanywa na migogoro ya kivita. Wataalamu hawa wana lenga kumaliza migogoro hii kwa njia ya utafiti wa kina, kukusanya takwimu na kuchapisha ikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo,na kusuluhisha migogoro.

Kituo hiki kikiongozwa na tunu kubwa  ya Haki na Amani ni chombo ambacho kina lenga kujenga amani ya kudumu Africa Mashariki, Africa ya Kati na Africa kwa ujumla tukianzia na Tanzania. Kituo hiki kimeanzishwa kushughulikia amani ambayo katika bara la Africa imekuwa kitu adimu. Kituo cha amani na migogoro ni namna nyingine ya kuzungumza na kujadili amani.
Kwa nini Tanzania kuwa na kituo kama hiki?
Tanzania ni mmoja katika nchi chache barani Africa sio tu kuwa ilipata uhuru wake kwa njia ya amani bila umwagaji wa wazi wa damu lakini pia ni mmoja kati ya nchi chache ambayo hajaingia katika utawala wa kidicteta, au wa kijeshi au kuwa na vita rasmi. Hii ni bahati kwa kuwa kuna baadhi ya nchi barani Africa ambazo tangu uhuru katika miaka ya sitini hazijawahi kuwa katika hali kama hiyo. Hata hivyo pamoja na upande huu mzuri, hapa Tanzania tumeanza kushuhudia viashiria ambavyo iwapo havitafanyiwa kazi mapema na kwa utaratibu wa kitaalamu tunaweza kujikuta katika hali ambayo nchi nyingi barani Africa zimejikuta. Hii inatokana na ukweli kuwa Amani ni tunu na kama ni tunu ni lazima itunzwe na ilindwe siyo kwa bunduki au kwa vurugu bali kwa haki na utulivu. Kuna viashiria vya wazi ambavyo vinaweza kuwa sumu ya kuvuruga amani ya nchi yetu.
Kwanza, ushindani wa kisiasa: Kuna kila dalili kuwa ushindani wa kisiasa unataka kufanyika kwa kutumia nguvu. Hii tunashuhudia pale tunapoona mikutano ya hadhara ikishambuliwa, kukitokea vurugu wakati wa mikutano ya kisiasa, hadi watu kupoteza maisha yao. Upinzani unavyozidi kuwa na nguvu vurugu nazo zinaonekana waziwazi.
Pili, ni suala la maliasili kama vile madini, ardhi, nishati za aina zote n.k. Barani Africa hiki ni chanzo kikuu cha vita. Hapa nchini tunashuhudia wananchi wakipambana na wawekezaji, wananchi wakipambana na serikali, kuna hali ya sintofahamu.
Tatu, wakulima na wafugaji. Ugomvi wa wakulima na wafugaji sio tu ule wa kimila wa zamani lakini sasa unaenda katika hatua ya juu zaidi ambapo kumekuwa na matokeo mabaya ya ugomvi huo.
Nne, ni suala la dini, ambalo hivi sasa linachukua sura nyingi. Kuanzia kujeruhiwa, hadi kuuuwa kwa wale ambao tunaweza kusema ni viongozi wa dini.


Haya matatizo tunayo hapa nchini na ukubwa wake na hatari yake kutoshughulikiwa kitaalamu inawezekana yasionekana leo lakini miaka michache ijayo tunaweza kuingia katika mgogoro ambao kuutatua itakuwa  ni kazi ngumu zaidi kuliko kuchukua  hatua sasa na kuzuia.
Hivyo basi Kituo cha amani na utafiti wa migogoro kinachukua hatua zifuatazo katika mipango yake:
1Elimu ya Amani ( Peace Education)
1.      .Utafiti, uandishi na uchapishaji
2.      Mafunzo mbalimbali kuhusu amani
3.      Mazungumzo, usuluhishi na ujengaji wa amani

Maeneo haya yatatekelezwa kwa njia zifuatatzo
a) Mafunzo na elimu
b) Semina na warsha
c) Ufuatiliaji na uhamashishaji
d) Kujenga uwezo
e) Kuvishirikisha vyombo vya habari katika kujenga amani

Tumesema kuwa ili kuzuia yale yanayoonekana hivi sasa hapa nchini kama hatari ya amani tunahitaji  kutumia mbinu za kitaalamu ambazo ni pamoja na elimu kwa umma lakini i pia kukazia kuwepo kwa sera za amani katika taasisi kama vile za elimu. Katika kuhamashisha amani tayari kituo cha amani na utafiti wa migogoro Africa kinashirikiana na Kituo cha Sheria na Haki za binadamu katika kutoa vipindi vya Radio na Televiisheni. Aidha tupo katika mazungumzo na Tume ya Taifa ya UNESCO kuhusu utoaji wa elimu ya amani katika taasisi na sekta za elimu. Ushirikiano huo upo katika hatua ya mazungumzo ambapo serikali itakuwa na nafasi yake. Pia katika mgogoro wa Mtwara kituo hiki kimetoa ushauri mbalimbali kuhusu mgogoro wa Mtwara.
Pia tumekuwa tikivishawishi vyuo vikuu hapa nchini kutoa elimu hii ya Amani katika ngazi mbalimbali. Tumeweza kutoa ushawishi huu kwa chuo kikuu cha Bagamoyo ambapo kuanzia mwezi wa kumi watakuwa na degrii ya udhamili ya “Peace Studies and Conflict Resolution”. Tunawahamashisha waandishi wa habari kuchukua kozi hii kwani itawapa mwanga mkubwa katika kutoa habari za migogoro mbalimbali. Vyuo vikuu vingine vipo vinajipanga katika kuanzisha kozi hii. Na haya ni matunda ya Kituo cha Amani na utafiti wa Migogoro Africa.
Sio tu tunalenga taasisi za elimu lakini pia tasnia nyingine kama za wasanii na wengineyo. Hivyo basi tuko mbioni kuanzisha tuzo mbalimbali za amani.
Kituo cha amani na utafiti wa migogoro Africa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali tutakuwa na tuzo ya amani kama ifuatavyo:
A)    Tuzo ya mwandishi wa habari  bora  na chombo cha habari bora kwa kuhamasisha amani,tukijua kuwa vyombo vya habari ni wadau wakuu wa amani.  
B)    Tuzo ya msanii bora wa muzuki ambaye atakuwa na wimbo wenye maudhui  ya amani na kukubalika katika jamii
C)    Tuzo ya mwanafunzi bora ambaye ataandika  insha inayohamasisha amani katika jamii.
Utaratibu wa kushiriki katika tuzo hizi utatangazwa hapo baadaye. Tuzo hizi zitakuwa zikitolewa kila mwaka wakati wa Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya Amani Duniani ambayo  huadhimishwa kila mwaka tarehe 21 septemba. Kituo cha amani na utatuzi wa migogoro kiko tayari kushirikiana na wadau wote wa amani ili kuhakikisha kuwa lugha ya mtanzania inakuwa siyo migogoro bali AMANI.
Kituo cha Amani na Utafiti wa Migogoro Afrika kina watakia AMANI katika kazi zenu.

Mtendaji Mkuu
Lioba Mpore.

No comments:

Post a Comment