Joseph Chibehe
National Sales Manager Tanzania Distilleries Ltd (+255 764 703 027 Ê È+255 767 266 601 P.O Box 9412 | Dar es Salaam | Tanzania, United Republic of joseph.chibehe@tz.sabmiller. |
Baadhi ya wananchi jijini Dar es Salaam,
wamepongeza hatua ya kundolewa bungeni kwa hoja
ya kupiga marufuku biashara ya Vinywaji vikali maarufu kama Viroba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, katika maeneo
mbalimbali ya starehe jijini Dar es Salaam jana,
walisema hatua hiyo imewafurahisha kwani
imewafanya sasa kuachana na uamuzi wa kurudia
kunywa tena pombe haramu ya gongo ambayo ni
hatari kwa afya zao.
Akielezea furaha yake, Adamu Mwaituka ambaye
alikutwa katika Baa ya Way Point eneo la Banana,
Ukonga, Dar es Salaam, alisema uamuzi huo
ameupokea kwa chereko kwani hicho kinywaji
anakipenda na kukitumia mara kwa mara.
Kwa upande wa mnywaji Fikiri Abdallah,ambaye
alikutwa akimimina viroba kwenye glasi katika Baa ya
Mama Seles, Banana, Ukonga, yeye alisema kuwa uamuzi
huo wa bunge kuacha kupiga marufuku viroba,
umemuokoa yeye na wenzie ambao afya zao
zilidorora walipokuwa wakinywa pombe haramu ya
gongo, lakini tangu waanze kunywa viroba miili yao
ina afya njema.
Akielezea athari mbazo zingetokea endapo, kinywaji
hicho kingepigwa marufuku, Suzan Amandus, mkazi
wa Ilala Mchikichini, alisema kuwa wengi wa watu
wenye kipato duni, wangenyimwa haki ya kutumia
kinywaji hicho na kurudia tena kunywa pombe
haramu zinazotengenezwa kienyeji.
Meneja wa Baa ya New Somba Park, iliyopo
Mwembeyanga, Temeke, Idrisa Chande, alisema
alifurahi sana baada ya kusikia hoja ya kupiga
marufuku viroba imesimamishwa, kwani wangefanya hivyo biashara
ingeyumba kwa vile wateja wake wengi ni watumiaji wa kinywaji hicho.
Hivi Karibuni ulizuka mjadala Bungeni, ambapo
baadhi ya wabunge wachache walitoa hoja wakati wa
kikao cha makadirio ya bajeti ya Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii, kuwa kinywaji aina ya kiroba kipigwe
marufuku wakidai kwamba aslimia kubwa ya
madereva hunywa na kusababisha ajali.
Akihitimisha hoja ya makadilio ya bajeti ya wizara
hiyo, Waziri wa Afya na Ustawi, Dk. Hussein Ali
Mwinyi, alisema kuwa hawawezi kutoa uamuzi juu ya
suala hilo mpaka watakapojadiliana kwa pamoja kati
ya wizara husika na wazalishaji wa vinywaji hivyo.
wamepongeza hatua ya kundolewa bungeni kwa hoja
ya kupiga marufuku biashara ya Vinywaji vikali maarufu kama Viroba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, katika maeneo
mbalimbali ya starehe jijini Dar es Salaam jana,
walisema hatua hiyo imewafurahisha kwani
imewafanya sasa kuachana na uamuzi wa kurudia
kunywa tena pombe haramu ya gongo ambayo ni
hatari kwa afya zao.
Akielezea furaha yake, Adamu Mwaituka ambaye
alikutwa katika Baa ya Way Point eneo la Banana,
Ukonga, Dar es Salaam, alisema uamuzi huo
ameupokea kwa chereko kwani hicho kinywaji
anakipenda na kukitumia mara kwa mara.
Kwa upande wa mnywaji Fikiri Abdallah,ambaye
alikutwa akimimina viroba kwenye glasi katika Baa ya
Mama Seles, Banana, Ukonga, yeye alisema kuwa uamuzi
huo wa bunge kuacha kupiga marufuku viroba,
umemuokoa yeye na wenzie ambao afya zao
zilidorora walipokuwa wakinywa pombe haramu ya
gongo, lakini tangu waanze kunywa viroba miili yao
ina afya njema.
Akielezea athari mbazo zingetokea endapo, kinywaji
hicho kingepigwa marufuku, Suzan Amandus, mkazi
wa Ilala Mchikichini, alisema kuwa wengi wa watu
wenye kipato duni, wangenyimwa haki ya kutumia
kinywaji hicho na kurudia tena kunywa pombe
haramu zinazotengenezwa kienyeji.
Meneja wa Baa ya New Somba Park, iliyopo
Mwembeyanga, Temeke, Idrisa Chande, alisema
alifurahi sana baada ya kusikia hoja ya kupiga
marufuku viroba imesimamishwa, kwani wangefanya hivyo biashara
ingeyumba kwa vile wateja wake wengi ni watumiaji wa kinywaji hicho.
Hivi Karibuni ulizuka mjadala Bungeni, ambapo
baadhi ya wabunge wachache walitoa hoja wakati wa
kikao cha makadirio ya bajeti ya Wizara ya Afya na
Ustawi wa Jamii, kuwa kinywaji aina ya kiroba kipigwe
marufuku wakidai kwamba aslimia kubwa ya
madereva hunywa na kusababisha ajali.
Akihitimisha hoja ya makadilio ya bajeti ya wizara
hiyo, Waziri wa Afya na Ustawi, Dk. Hussein Ali
Mwinyi, alisema kuwa hawawezi kutoa uamuzi juu ya
suala hilo mpaka watakapojadiliana kwa pamoja kati
ya wizara husika na wazalishaji wa vinywaji hivyo.
No comments:
Post a Comment