header

nmb

nmb

Friday, May 17, 2013

CHAZ BABA AMVISHA PETE YA UCHUMBA REHEMA SOSPETER.


Charles Gabriel ‘Chaz Baba,’ akimvisha pete mchumba’ke, Rehema Sospeter.
Tukio hilo lililoshuhudiwa na Amani lilijiri Mei 11, mwaka huu ndani ya Ukumbi wa Business Park, Kijitonyama, Dar, wakati bendi yake ilipokuwa ikitambulisha albam mpya, Risasi Kidole.
Akizungumza na paparazi wetu mapema wiki hii, Chaz Baba alisema ameamua kuonesha uamuzi wake huo kuanzia kwa mashabiki wake waliofika ukumbini na kwa wale wasiofika kwa sababu wengi wao walikuwa hawamuamini.
“Nilifanya vile kukata vilimilimi ‘coz’ tangu nimegawa kadi za mchango wa harusi, kumekuwa na maswali mengi ambayo yanaashiria wengi hawaamini uamuzi wangu,” alisema Chaz.

No comments:

Post a Comment