header

nmb

nmb

Wednesday, February 27, 2013

Mataperi watua mji wa iringa

  

Mkuu  wa mkoa wa Iringa Dkt Christine Ishengoma

Wimbo la utapeli limevamia kwa kasi ya ajabu katika mkoa  wa Iringa baada ya  wananchi kutapeliwa kupitia ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Terresia Mahongo na mkuu  wa mkoa  wa Iringa Dr Christine Ishengoma .

Matapeli hao  wamekuwa  wakiwapigia  watu mbali mbali simu kuwa katika  ofisi ya mkuu wa mkoa na mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa kuna pikipiki zimetolewa na Rais Jakaya  kikwete kwa ajili ya maofisa ugani na kuwa wao wamebahatika kuzipata mbili  hivyo wameamua kuziuza kwa bei ya Tsh milioni 2.5 na kama mteja anahitaji afike ofisi za Manispaa na kwa mkuu  wa mkoa kulipa  pesa hiyo ili  apewe pikipiki na hati yake.


Hata hivyo inadaiwa kuwa baada ya  wateja kufika hapo  wamekuwa wakiambiwa  watoe  pesa hiyo nje ya ofisi na  wakatafute usafiri wa kubeba pikipiki hizo na ndipo  wanapoingizwa mjini kwa matapeli hao  kukimbia na kuwaacha wakishangaa .

Matukio hayo yametokea kwa nyakati tofauti katika uzio wa ofisi za Manispaa ya Iringa na ofisi ya mkuu  wa mkoa ambapo watu  watatu  wametapeliwa akiwemo  kijana mmoja wa Kiwere aliyetapeliwa kiasi cha  shilingi 200,000 na ushehe za mauzo ya nyanya kwa matapeli  hao kujifanya  ni maofisi wa polisi ambao wanafanya msako  wa fedha  za mzungu  zilizoibwa jana na kukagua fedha za kila mwananchi na  hivyo kutaka fedha za mkulima huyo kuchunguzwa huku yeye akisubiri nje ya ofisi za Manispaa ya Iringa kabla ya matapeli hao  kutokea mlango wa  pili na kukimbia

No comments:

Post a Comment