header

nmb

nmb

Friday, August 3, 2012

HIVI NDIVYO ADEN RAGE ALIVYOWAPIGA BAO YANGA NA KUMSAINI MBUYI TWITE

Wakati makamu mwenyekiti wa Simba Geodfrey Nyange Kaburu na mwenyekiti wa kamati ya usajili Zakaria Hans Pope wakiwa wanamalizana na kiungo mshambuliaji Mrisho Khalfan Ngassa na mabingwa wa Tanzania bara, upande mwingine mwenyekiti wa klabu hiyo Mheshimiwa Aden Rage nae alisafiri umbali wa kilomita zipatazo 1,459.7, kutoka Dar kwenda Kigali kukamilisha usajili wa beki wa kati wa APR Mbuyi Twite.

Wakati Rage akiwa anamsainisha Twite ambaye pia alikuwa akiwindwa na mabingwa wa Africa mashariki na kati Yanga - upande mwingine Ngassa alikuwa anatia saini kuitumikia Simba kwa miaka 2.

Kwa maana hiyo Simba wakawa wameipiga bao wapinzani wao Yanga ambao wao pia walikuwa wakiwahitaji wachezaji hao wote wawili Twite na Ngassa.

Na haya ndio matambo ya Simba kupitia msemaji wao Ezekiel Kamwaga kuhusu kuwapiga bao wapinzani wao.

No comments:

Post a Comment