header

nmb

nmb

Tuesday, September 27, 2011

BALOZI WA BRAZIL

Balozi wa Brazil nchini Tanzania Bw. Fransisco Luz amesema, Serikali ya Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi kwa upana wake ila inahitajika kufanya kazi ya ziada kuhakikisha inatengeneza nafasi nyingi za rasilimali watu ambalo ndilo tatizo kubwa linalopelekea nchi kuyumba kiuchumi na wananchi wake wengi kuendelea kuwa maskini.

Balozi Huyo aliyasema hayo katika mahojiano maalum yaliyofanyika kwenye ofisi za Balozi huyo zilizopo maeneo ya Oysterbay jijini Dar es salaam, mwandishi wa habari hii alitaka kufahamu maandalizi ya ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda , anayetarajiwa kufanya ziara ya siku SITA Nchini BRAZIL kuanzia mwanzoni mwa Mwezi ujao.

Balozi LUZ alisema, Kutokana na nchi ya Tanzania kuwa na Rasilimali nyingi akitolea mfano GESI ya ASILI,Makaa ya Mawe na Mafuta ambayo yako katika mchakato wa kutafutwa kupitia kampuni kutoka nchini Brazil, katika maeneo ya bahari ya hindi, Tanzania itaweza kufanikiwa kwa kiwango cha juu katika kukuza uchumi wake pamoja na kuwawezesha wakulima wadogo wadogo ambao ndiyo wainua uchumi wa nchi.

Akizungumzia suala la Rasilimali watu, aliishauri Serikali kuanzisha vyuo AU Kushirikiana na vyuo vikuu vitakavyotoa elimu ya juu katika kuwezesha kutoa wahitimu wenye sifa za kufanya kazi katika sekta za Nishati akitolea mfano shughuli itakayohitaji wahandisi wengi wa uchimbaji mafuta katika kipindi kijacho.

Kuhusu Safari ya Mheshimiwa waziri Mkuu,Balozi LUZ amesema, Katika ziara hiyo mheshimiwa waziri anatarajiwa kutembelea maeneo mbalimbali ya kuvutia na yatakayoleta tija kwa nchi ya Tanzania, zikiwemo sekta za kilimo kwasababu kilimo Kwanza ndiyo kipaumbele cha nchi, pia atatembelea maeneo ya mifugo, Miundombinu pamoja na miradi ya mbalimbali ya maendeleo nchini humo sambamba na kukutana na wafanyabishara wenye nia ya kuwekeza Tanzania na muungano wa vyama mbalimbali.

Sambamba na hilo balozi huyo wa Brazil amesema, Waziri Mkuu pia katika ziara hiyo atakutana na Makamu wa Rais wa nchi hiyo, Waziri Mkuu, Waziri wa Mambo ya Nje wa Nchi ya Brazil pamoja na mawaziri wengine.

Katika ziara hiyo Waziri Mkuu PINDA , ataongozana na msafara wa Viongozi kadhaa kutoka hapa nchini Akiwemo waziri wa Nishati na Madini Bw.William Ngeleja, Waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu uwekezaji na uwezeshaji Dr. Mary Nagu pamoja na viongozi wengine wa juu wa serikali .



No comments:

Post a Comment