header

nmb

nmb

Wednesday, January 27, 2010

RAISI WA LIBERIA ANOGEWA!


Ellen Jonson

RAIS wa nchi hii, Ellen Johnson Sirleaf ametangaza hazima yake ya kugombea kwa mara ya pili, licha ya awali kuahidi kutumikia nafasi hiyo kwa kipindi kimoja cha miaka sita.
Rais huyo mwenye umri wa miaka 71 amesema kuwa kutangaza hazima yake mapema ni kutaka kumaliza dhana zinazotolewa juu ya nia yake ya kugombea mwaka 2011.


Msemaji wa rais huyo, Cyrus Badio amesema kabla ya kutangaza hazima hiyo awali hakugundua kama kulikuwa na kazi kubwa ya kutekeleza kabla ya mwaka 2005, katika nchi inayojaribu kurejesha hali yake ya awali baada ya kuwepo kwenye vita kwa muda mrefu.


Hellen ni mwanamke wa kwanza kuchaguliwa kuwa Rais barani Afrika baada ya kushinda kwa asilimia 59 ya kura zote katika marudio ya uchaguzi dhidi ya mchezaji soka maarufu, George Weah.



Katika uchaguzi huo wa kwanza Weah alipata kura nyingi katika duru ya kwanza ya uchaguzo huo uliofanyika baada ya kumalizika vita ya wenyewe kwa wenyewe mwaka 2003.
"Kwa leo nafahamu mahali tulipo, nafahamu mahali tunapotakiwa tuwepo kesho na ninafahamu tutafikia mahali hapo,"Hellen aliwaeleza wabunge ambao walikuwa wakisikiliza hotuba yake ya mwaka.


Mwandishi wa Shirika la Utangaazaji la Uingereza, BBC, Jonathan Paye-Layleh aliyepo mjini hapa ameripoti kuwa tangazo la kiongpozi huyo linaweza kupokelewa kwa mikono miwili na wafuasi wake lakini akasema kuwa hali hiyo inaweza kuwa tofauti kwa wapinzani.
Charles Brumskine, who came third in the 2005 presidential poll, said he was concerned about Mrs Johnson-Sirleaf's age.


"Mrs Sirleaf has done what she could do, I think she's reached the limit of her capacity," he told the BBC's Network Africa programme.

No comments:

Post a Comment