header

nmb

nmb

Thursday, September 26, 2013

KUNDI LA Cash Money, RATOA MSAAA KWA WAGOJWA HOSPITALI YA TEMEKE


Wana kikundi cha Cash Money wakiwa tayali kwa kutoa msaada katika hospitali ya Temeke
Mlezi wa Kikundi cha Cash Money ,Ratifa Masasi kulia akimkabibi muhuguzi wa wodi ya watoto bi, Nuswe Ambokile zawai mbalimbali walizoleta kwa ajili ya watoto waliolaza katika hospital ya Temeke





Na Mwandishi Wetu
MSANII nguli wa muziki wa dansi aliyestaafu, Muhidini Gurumo, atapanda
jukwaani leo kutumbuiza na mkewe, sambamba na kupewa zawadi za
heshima.

Gurumo atatoa  burudani hiyo ikiwa ni sehemu ya kuwaaga mashabiki,
ambapo shughuli hiyo itaambatana na uzinduzi wa kundi la Cash Money,
la Tandika mjini Dar es Salaam.

"Tumeandaa zawadi kwa mzee Gurumo kutokana na heshima kubwa aliyonayo
katika tasnia ya muziki na kujenga maadili kwa taifa kutokana na
nyimbo zake.

Hivyo zawadi zetu zitaenda sambamba na uzinduzi, ambapo tumepanga
hivyo, ili lee mwenye chochote ampe mzee wetu,"Aliongeza Latifa Masasi
mlezi wa kundi hilo.

Uzinduzi huo unafanyika kwenye ukumbi wa Equator Grill, Mtoni kwa Aziz
Ali, Dar es Salaam na utapambwa na bendi mbalimbali za taarabu
zikiwemo Coast na G Five.

Kundi la Cash Money ambalo lilianzishwa mwaka 2011, pia limetoa vitu
mbalimbali kwa wodi ya watoto, na vituo vya watoto yatima jana, ikiwa
ni sehemu ya uzinduzi huo


Baadhi ya wanachama wa kikundi cha Cash Money wakimfariji Bi Naomi Ramadhani
Msanii wa bendi ya Msondo ngoma Saddy Ally katikati akisalimiana na wanakikundi cha cash money walipokutana katika hospitali ya Temeke wakitokea kutoa msaada


Mlezi wa kikundi cha cash money bi, Ratifa Masasa akimfariji mtoto Salimu Ally wakati walipokwenda kutoa msaada katika hospitali ya temeke dar es salaam mwingine ni mama mtoto Tabu Salumu mkadhi wa Tandika

No comments:

Post a Comment