Kwa bahati mbaya kuna Wabongo wana roho mbaya, na mbaya zaidi wanaweza kukuendea kwa mganga hata kijijini kwao ili tu usifanikiwe. Lakini pia kuna ndugu huko kijijini kwenu ukienda kuwatembelea linakuwa kosa, wanaamua kukupiga kitu mambo yako hapa mjini yanakwama kishenzi. Nimekusanya hapa baadhi ya mambo ambayo ukiona tu yameanza kukuandama ujue kijijini kwenu wamekuendea kwa mganga;
i. Ukiona kila unapodownload kitu ikifikia 99% hakiendelei ujue tayari
ii. Ukiona umenunua Blackberry kwa shilingi laki 7, kesho yake unakuta duka jingine wanauza ileile kwa shilingi laki 3 na nusu ujue wameshakushughulikia
iii. Ukiona hata ukitumia pafyumu gani, kikwapa kiko palepale ujue tayari
iv. Ukiona watu wote wanatanua, na wewe ukafuata ukajikuta unakamatwa peke yako ujue wameshafanya mambo kijijini kwenu
v. Unaingia chumba cha intaview unajikuta umesahau hata jina lako, hapo ujue tayari
vi. Ukikosea ukajikuta umetumia super glue badala ya matone ya dawa ya macho, hapo wameshakutwanga
vii. Unakuta mchwa wamekula jina lako tu kwenye vyeti vyako vya shule we nione jamaa wameshakuchapa
DREVA SIMAMISHA
Mlevi alipanda daladala akiwa anatoka Msasani anaelekea kwake Ubungo, mara simu ya mdada jirani yake ikalia;
MDADA: Hellow, Sweety mambo? Niko kwenye daladala naelekea Kiwalani kwa shangazi kuna msiba ntakutafuta nikifika. Baada ya muda simu ya mtu mwingine ikalia;
JAMAA: Hello, aise nivumilie hapa niko kwenye basi naelekea Ifakara nikirudi ntakupa mzigo wako. Simu ya konda ikalia,
KONDA: Vipi mshikaji, leo noma mwanangu, nimepata zali hapa napiga mzigo niko daladala la Mwenge Kunduchi.
MLEVI: Dreva simamisha gari nataka kushuka maana sijui hili gari linelekea wapi
MDADA: Hellow, Sweety mambo? Niko kwenye daladala naelekea Kiwalani kwa shangazi kuna msiba ntakutafuta nikifika. Baada ya muda simu ya mtu mwingine ikalia;
JAMAA: Hello, aise nivumilie hapa niko kwenye basi naelekea Ifakara nikirudi ntakupa mzigo wako. Simu ya konda ikalia,
KONDA: Vipi mshikaji, leo noma mwanangu, nimepata zali hapa napiga mzigo niko daladala la Mwenge Kunduchi.
MLEVI: Dreva simamisha gari nataka kushuka maana sijui hili gari linelekea wapi
KAOGEEEEEEEE
Ukiwashwa kiganja wanasema utapata pesa, ukiwashwa jicho wanasema kuna mtu anakuteta. Ukiwashwa sehemu za siri ujue hizo fungus..kaogeeeeeeeeeeee







No comments:
Post a Comment