header

nmb

nmb

Thursday, January 24, 2013

Skylight Band yazidi kupasua anga za kimataifa katika muziki wa live Band jijini Dar es Salaam

Mmoja wa wapiga vyombo wa Skylight Band akionyesha kipaji chake cha kusakata sebene.
 Ukawadia ule muda wa mduara na mambo yalikuwa kama hivi.....
 Wema Sepetu na Zamaradi Mketema wakiserebuka.
 
 Mdau akaomba kupata ukodak na warembo hao.
Mariam Nnauye na TID.
Mdau Benjamin katika pozi na mtoto wa ukweli.
Aneth Kushanba AK47 akiongoza safu ya vijana wa SKYLIGHT Band kutoa burudani kwa mashabiki wake Ijumaa iliyopita kwenye kiota cha maraha Thai Village Masaki Jijini Dar. Bendi hiyo inapiga hapo kila siku za Ijumaa kuanzia Saa 3 usik

MPAMBANO WA MASUMBWI KUPIGWA Janual 27 katika ukumbi wa wa CCM Tandare

SUPER D BOXING COACH


Mabondia Hassan Mandulla na Jems Martin wanatarajia kupanda ulingoni Janual 27 katika ukumbi wa wa CCM Tandare Dar es salaam akizungumza mpambano huo mwandaaji Waziri Rosta
amesema kutakuwa na mapambano mengine ya utangulizi yakiwemo ya mabondia maarufu na chipkizi alisema mapambano ya utangulizi ni Fadhiri Majia na Anton Matiasi mpambano mwingine

Utawakutanisha Shabani Kilumbelumbe na Mwaite Juma na Chaeles Mashali atavaana na Adam Ngange, Julias Noro atapambana na Abdallah Luwajempambano mwingine utawakutanisha Rajabu Tumaini na Daudi Anton na Rashid Mohamed Atavaana na Eliman Richard wakati Rashid Hamisi atamvaa Omary Shabani


Super D, alisema katika mpambano huo atasambaza DVD zake mpya tofauti na kanda yake ya awali iliyokwenda kwa SUPER D BOXING COACH, DVD za sasa zimeandaliwa kisasa na zikiwa na mchanganyiko wa ‘clips’ za michezo ya nyota wa Dunia katika kuwafunza watu namna ya kupigana ngumi.Super D, alisema mbali na michezo ya nyota hao wa Dunia akiwemo Manny Pacquio,Juan Emanuel Marquez, Floyd Maywether, Roy Jones na wakali wengine DVD hizo zina.

 michezo
ya tamasha lao la ngumi wanaloendesha kwa kushirikiana na kocha mkongwe Habibi Kinyogoli.”katika muendelezo wa kuwafunza watu ngumi kwa njia rahisi, nimetoa dvd pamoja na CD nyingine tofauti zilizokusanya michezo ya mabingwa wa dunia na mafunzo ya ngumi tunayoendesha kupitia tamasha letu na Kinyogoli Foundition ” alisema.
 Super D ambae ni kocha wa timu ya ngumi ya Ashanti pamoja na timu ya mkoa wa Ilala kimichezo alisema anamini kupitia njia  hii watu wengi wenye kupenda kujifunza mchezo wa ngumi kwa kuangalia mbinu na ufundi katika mchezo huo kupitia michezo ya mabondia waliopo kwenye dvd hizo.  
Aliongeza kuwa, mbali na dvd hizo bado wanaitajika vijana wenye vipaji kujitokeza kuja kushiriki katika mazoezi ya ngumi ili wajiunge na wenzao wa
timu ya Ashanti na Amana kujifunza ‘live’ chini ya makocha Habibu Kinyogoli, Kondo Nassoro, na yeye mwenyewe Super D na wengine wanaowanoa vijana

MATOKEO KIDATO CHA PILI YATANGAZWA

Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillipo Murugo (katikati), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari, Dar es Salaam, alipokuwa akitangaza matokeo ya kidato cha pili nchini.

Mkurugenzi wa Shule za Sekondari, Charles Phillemon akifafanua jambo wakati wa kutangaza matokeo hayo ya kidato cha pili. Kulia ni Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Phillipo Murugo

NA MAGRETH KINABO – MAELEZO
SERIKALI imesema kwamba kuanzia mwaka huu imerudisha hadhi ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Pili, hivyo mwanafunzi atakayepata wastani wa chini ya asilimia 30 hataruhusiwa kuendelea na kidato cha tatu, bali ataruhusiwa kukariri darasa mara moja tu.
Imefafanua kuwa mwanafunzi atakariri na kushindwa kufikia wastani wa asilimia 30 ataondolewa ataondolewa katika mfumo rasmi wa elimu. Mbali na hilo imesema ina mpango wa kuurudisha hadhi mtihani wa darasa la nne, hivyo itatoa maelekezo muda si mrefu baada ya kumalizika kwa uchunguzi.
Aidha imeongeza kuwa wazazi na walezi watapaswa kuchangia gharama za za uendeshaji wa mitihani hiyo ikiwemo mingine ya kitaifa ya kidato cha nne na sita kuanzia mwaka huu.
Kauli hiyo ilitolewa leo na Naibu Waziri wa Elimu, Philipo Mulugo wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dares Salaam kuhusu tamko la serikali kuhusu kupandishwa kwa hadhi ya mitihani hiyo na gharama za uendeshaji wa mitihani ya taifa.
“Kuanzia leo tunarudisha hadhi yake,” alisema Waziri Mulugo.
Alisema hatua hiyo imefikiwa baada ya kufanyika uchunguzi uliofanyika mwaka jana kubaini kuwa moja ya sababu zilizochangia ufaulu duni wa wanafunzi wa kidato cha nne, mwaka 2010 ni kutokana na kuwaruhusu wanafunzi kuendelea na masomo hata baada kushindwa kufikia alama ya ufaulu.
Uchunguzi Ulifanyika baada ya Bunge la Jamhuri la Muungano wa Tanzania kuagiza serikali na wadau wengine kufuatilia chanzo cha kushuka kwa ufaulu huo.
Waziri Mulugo alisema ufaulu wa kidato cha pili umekuwa ukishuka kuanzia mwaka 2008 hadi mwaka 2010 hivyo kuashiria wanafunzi na walimu kutofanya bidii za makusudi katika kujifunza na kufundisha.
Akizungumzia kuhusu uchangiaji wa elimu wa gharama za uendeshaji wa mitihani ya Taifa alisema uendeshaji wa mtihani umekuwa mgumu kufutia ongezeko la gharama za uendeshaji linaloendana sambamba na ongezeko la idadi ya shule pamoja na wanafunzi mwaka hadi mwaka, ambapo alitolea mfano wa mtihani wa kidato cha pili gharama za zake ni sh. bilioni sita wakati wa kidato cha nne ni sh bilioni 27.9.

Alisema katika mtihani huo wazazi na walezi watakiwa kuchangia sh. 10,000 kwa kila mwanafunzi kwa shule za serikali na zisizo za serikali.
Kwa upande wa mitihani ya kidato cha nne na sita wazazi na walezi watapaswa kuchangia sh .35,000 kwa kila mwanafunzi kwa shule za serikali na zisizo za serikali.
Katika hatua nyingine Waziri Mulugo alisema serikali inatarajia kutangaza ajira za walimu wa msingi na sekondari mwezi huu , na hivi karibuni itatangaza matokeo ya mtihani wa kidato cha pili.
Hii ni ni mara ya pili kwa serikali kurejesha mtihani wa kidato cha pili mara ya kwanza ilikuwa mwaka 1999 tangu ulipoanzishwa mwaka 1984
u.

No comments:

Post a Comment