header

nmb

nmb

Tuesday, March 30, 2010

MAZISHI YA ALIYEWAHI KUWA RPC MSAIDIZI KAMANDA SSP,MACHA



SSP ,MACHA AKIWA OFISINI ENZI ZA UHAI WAKE.KWA SASA ALIKUWA NI MSTAAFU

HISTORIA YA MAREHEMU HERI MACHA


WASIFU
Marehemu alizaliwa Tarehe 23/09 /1941 katika kijiji cha Kondeni.

ELIMU:
Alianza shule ya Msingi Kirua 1948 na baadaye alihamia Lutheran Middle School Lyakrim na kuhitimu darasa la Nane October 1956
1957 alijiunga na “AFRICA HIGH SCHOOL KYEBANDO – UGANDA” Ambapo alipata Certificate ya JUNIOR SECONDARY THREE LEAVING EXAMINATION.”

KAZI
1960 Aliajiriwa na kampuni ya ELEMENTARY TYPE WRITING hadi 1961, tarehe 11 / 1963 alijiunga na Chuo cha polisi (CCP) na kuhitimu kozi 01 / 06 / 1963 na kuanza kazi rasmi. 1967, katika mwaka huo alipandishwa cheo na kuwa ASSISTANT INSPECTOR nakudumu katika cheo hicho alidumu katika cheo hadi 1974 ,kutokana na Uadilifu wake mwaka huo huo alipandishwa cheo na kuwa FULL INSPECTOR akiwa Wilaya Korongwe mkoani Tanga.

Marehemu Macha alipandishwa cheo na kuwa SSP cheo alichodumunacho mpaka alipo staafu Jeshi 1997 akiwa Mkoani Kilimanjaro.

Baada ya kustaafu Mzee Macha alirudi Kijijini kwake nakuendelea na shughuli za Kilimo hadi mauti ilipomkuta mwaka huu.
MAISHA YA NDOA
1963 marehemu alijaliwa kufunga ndoa n kupata watoto 6 watatu wakiwa wa kiume na watatu ni wakike .
KUUGUA. Na Mauti


Marehemu alianza kuugua Mwaka 1988 akiwa mkoani Tanga hali iliyopelekea afanyiwe upasuaji wa tumbo katika Hospitali ya Rufaa KCMC. Baada ya upasuaji huo Marehemu aliendelea kusumbuliwa na shinikizo la damu pamoja na ugonjwa wa Gout ambayo ilimfanya atibiwe katika hospital mbalimbali za Mkoa hadi mauti yalipomfika tarehe 24 / 03 / 2010, saa 5.30 usiku.

Marehemu ameacha Mjane, watoto 6 na wajukuu 8.

SHUKURANI:

Shukurani zetu za dhati ziwaendee Madaktari, manesi na wahudumu wote wa KCMC na hospitali zote za Mkoa ambazo Mzee aliwahi kutibiwa kwa lengo la kujaribu kuokoa uhai wake. Shukurani za pekee ziwaendee Mapadri / Wachungaji na wote waliotoa huduma za Kiroho, Pia wakwezake Mr Kaaya ,Mr Faki,na Mr Patrick,

Waombolezaji wakiwa wamebeba mwili wa Kamanda Macha


Mke na Watoto wa Kiume wakiomboleza


Katika Majonzi mazito na huzuni kubwa ni mama yetu mke wa marehem Mrs Macha,kushoto. na watoto wake


Mtoto wa marehemu mama Sundey na mjukuu wa marehem Sundey wakiwa katika majonzi makubwa wakati wa kuaga mwili wa Mzee Macha

Baadhi ya ndugu na Jamaa kutoka mkoa wa Tanga ambako Mzee Macha aliwahi kufanya kazi wakiwa katika maombolezo.



HAWA NI WAKWE WA MAREHEMU MACHA,KUTOKA KUSHOTO NI MR. FAKI NA MWANA prhabari.blogspot.com


Mtoto wa Marehem kulia. Merry Macha na Mjomba wa Marehem Stella G.Masue

Tumpambe Baba yetu Mungu amekupenda zaidi yetu

No comments:

Post a Comment